Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeadhimisha siku ya Viwango Dunia
kwa kutoa zawadi na vyeti kwa wanafunzi walioshinda shindano la
uandishi wa Insha kama sehemu sehemu ya maadhimisho hayo na pia
kuwajengea uwezo na uelewa wanafunzi juu ya umuhimu wa viwango. Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Prof.Egid
Mubofu alisema shirika lake linaipa siku ya viwango duniani kwa
kuwajengea uwezo vijana kwa kuwashindanisha kwenye uandishi wa insha.
“Lengo kubwa la maadhimisho haya ni kutoa elimu kwa wananchi juu ya
umuhimu wa viwango katika kuboresha maisha ya wananchi katika ubora wa
vitu vyao, afya , usalama na biashara,” alisema Prof.Mubofu
Prof. Mubofu alisema kila mwaka Shirika la Viwango Duniani huwa na
Kauli mbinu yake ambayo kwa mwaka huu ni “Viwango huifanya Miji kuwa
ya Kisasa zaidi” ambapo kauli mbiu hii inaweka msisitizo kupitia
viwango uboreshaji wa maisha ya wakazi wa mijini kuwa ya kisasa zaidi.
“Shirika huandaa mashindano ya Insha katika shule za sekondari
kupitia kauli mbinu ya mwaka ya viwango lengo ikiwa kupima uwezo wa
wananfunzi katika ufahamu wao kuhusu viwango,” alisema Prof.Mubofu
Alisema hii inatoa nafasi ya kupima kwa namna gani wananchi
wanaelewa juu ya umuhimu wa viwango na kipi kifanyike katika
kuwajengea uwezo hasa wanafunzi katika kuelewa juu ya majukumu na
umuhimu wa viwango katika maisha yao.
Prof.Mubofu alisema TBS imetoa zawadi pamoja na vyeti kwa washindi wa
insha ikiwa ni motisha ilikuchochea ushiriki wa wanafunzi wengine
katika mashindano mbalimbali yanayotolewa na shirika kuhusu umuhimu wa
viwanda.
Aliongeza kuwa kutoka na ushiriki wa wanafunzi katika shindano hilo
kuwa mkjubwa, TBS imejipanga kuboresha vigezo vya ushiriki ili kutoa
nafasi kwa wanafunzi wa ngazi zote kushiriki kikamilifu.
“ TBS imejipanga kuboresha maisha ya watanzania kwa kusimamia viwango
vya ubora katika maeneo yote hasa uzalishaji na ujenzi na afya,”
alisema Prof.Mubofu na kuongeza kuwa azma ya serikali ya awamu ya tano
ya kuwa nchi ya uchumi wa kati na viwanda itatekelezeka kwa kuwa na
usimamizi madhubuti wa viwango.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa uandaaji viwango TBS, Bi. Edna Ndumbaro
alisema matumaini ya TBS kupitia mashindano ya insha katika
maadhimisho ya siku ya viwango duniani ni kuwapatia uelewa na elimu
kuhusu maswala ya viwango kwa manufaa ya sasa na jamii ijayo.
“Wanafunzi 10 kutoka Shule za sekondari za Kibaha,Feza, Elboru na
Loyola walipatiwa zawadi ikiwa ni ishara ya kuifanya elimu ya viwango
kuwa endelevu,” alisema Bi.Ndumbaro
Mshindi wa kwanza wa shindano la Insha alikuwa mwanafunzi kutoka shule
ya Sekondari Kibaha,Bw. Barnabas Michael ambaye alisema kushiriki
kwenye mashindano kunamfanya mwanafunzi kujijengea uwezo wa kujieleza
na pia kuwa na ufahamu wa mambo kwa mapana yake.
“Wito wangu kwa wanafunzi wenzangu ni kujitokeza kwa wingi kushiriki
katika mashindano mbalimbali kwani yanasaidia kuongeza maarifa na
uwezo wa kupambanua mambo mbalimbali,” alisema Bwana Michael
Siku ya Viwango Duniani uazimishwa kwa lengo la kuelimisha juu ya
uelewa miongoni mwa mamlaka za udhibiti, viwanda na walaji kuhusiana
na umuhimu wa viwango kwa uchumi wa dunia ikiwepo Tanzania.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania(TBS) Prof.Egid Mubofu akitoa mada kwenye hafla ya maadhimisho ya Siku ya Viwango Duniani yaliyofanyika katika ofisi za shirika hilo Ubungo jijini Dar salaam. Katika maadhimisho hayo yaliambatana na utoa wa vyeti na zawadi kwa wanafunzi walioshinda katika shindano la uandishi wa insha uliendana na kauli mbiu ya maadhimisho ambayo ni “VIWANGO HUIFANYA MIJI KUWA YA KISASA ZAIDI”
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania(TBS) Prof.Egid Mubofu akikabidhi zawadi ya Laptop, cheti na Kiasi cha shilingi laki tatu na nusu kwa mshindi wa Kwanza wa uandishi wa Insha mwanafunzi Shule ya Sekondari Kibaha Bw. Barnabas Michael katika shindano maalum la kuadhimisha siku ya viwango Duniani ikiwa na kauli mbiu “VIWANGO HUIFANYA MIJI KUWA YA KISASA ZAIDI” . shindano hilo limelenga wanafunzi kwa lengo la kuandaa kizazi chenye uwelewa wa kutosha juu ya umuhimu wa viwango katika ubora, Afya, Usalama na Biashara.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...