Mfanyakazi wa Kampuni ya mtandao wa simu ya Zantel Kitengo cha Ugavi Bi. Mainda Madiwa Chanika akichangia damu kwa hiari wakati wa zoezi la uchangiaji damu salama lililowahusisha wafanyakazi wa kampuni hiyo ikiwa ni njia ya kukabiliana na wingi wa watu wengi wenye uhitaji wa huduma hiyo kila mwaka. Zoezi hilo lilifanyika mwishoni mwa juma katika makao makuu ya Kampuni hiyo jijini Dar es salaam. (Kushoto) ni Mwakilishi kutoka Mpango wa Taifa wa damu Salama-Kanda ya Mashariki Bi. Cecilia Meena.
Afisa Uhamasishaji kutoka Mpango wa Taifa wa damu Salama-Kanda ya Mashariki Bi. Fatuma Mjungu akizungumza na vyombo vya habari wakati wa zoezi la uchangiaji damu kwa hiari ili kuokoa maisha ya watanzania wengine lilowahusisha baadhi ya wafanyakazi wa Zantel lililofanyika mwishoni mwa juma katika makao makuu ya Kampuni hiyo jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Mauzo ya jumla wa Kampuni ya Zantel, Deo Ngonyani akishiriki katika zoezi la uchangiaji damu salama lililowahusisha wafanyakazi wa kampuni hiyo ikiwa ni njia mojawapo ya kuokoa maisha ya watanzania wenye uhitaji mkubwa wa huduma hiyo. Zoezi hilo lililifanyika mwishoni mwa juma katika makao makuu ya Kampuni hiyo jijini Dar es salaam. (Kulia) ni Mwakilishi kutoka Mpango wa Taifa wa damu Salama-Kanda ya Mashariki Bi. Cecilia Meena.
Mfanyakazi wa Kampuni ya mtandao wa simu ya Zantel Kitengo cha Uhasibu Bw. Ally Abdallah akichangia damu kwa hiari wakati wa zoezi la uchangiaji damu salama lililowahusisha wafanyakazi wa kampuni hiyo ikiwa ni njia ya kukabiliana na wingi wa watu wengi wenye uhitaji wa huduma hiyo kila mwaka. Zoezi hilo lilifanyika mwishoni mwa juma katika makao makuu ya Kampuni hiyo jijini Dar es salaam. (Kushoto) ni Mwakilishi kutoka Mpango wa Taifa wa damu Salama-Kanda ya Mashariki Bi. Cecilia Meena.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...