SERIKALI imeahidi kutoa pembejeo za kilimo cha kisasa yakiwemo matrekta kwa ajili ya kuwawezesha wanawake kupitia taasisi inayojihusisha na kuendeleza wanawake katika kilimo Tanzania (CAWAT) ili waweze kushiriki kikamilifu katika kilimo cha kisasa hususani cha kibiashara.

Ahadi hiyo ya Serikali ya serikali imetolewa na Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi William Ole Nasha kwa Niaba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati akizungumza kwenye harambee kukusanya fedha kwa ajili ya kuwezesha mradi wa kuwajengea uwezo wanawake waweze kushiriki kikamilifu katika kilimo biashara iliyoandaliwa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Land O’ Lakes kwa kushirikiana na CAWAT na kufanyika jijini Dar es salaam mwshoni mwa wiki.

“Serikali ipo tayari kutoa pembejeo hizo za kilimo cha kisasa yakiwemo matrekta bora kabisa ambayo yataolewa kwa vikundi vya kina mama wanachama wa CAWAT ambao wataonyesha nia na uwezo wa kutekeleza kilimo cha kisasa hususani cha kibiashara. Zaidi wanufaika hao watahakikishiwa soko la uhakika kwa kile watakachozalisha,’’ alisema Ole Nasha ambae pia yeye binafsi alitoa mchango wa mil. 2 kwenye harambee hiyo.

Alisema serikali ipo tayari kushirikiana na taasisi yeyote nchini yenye nia ya dhati katika kuleta mabadiliko yenye tija yatakayoliwezesha taifa kuongeza kasi yake katika kuelekea uchumi wa viwanda na mapinduzi ya kilimo.  
 Mkurugenzi Mradi kutoka taasisi ya Land O’ Lake Dr Rose Kingamkono akizungumza kwenye harambee ya kukusanya fedha  kwa ajili ya kuwezesha mradi wa kuwajengea uwezo wanawake waweze kushiriki kikamilifu katika kilimo biashara iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
 Baadhi ya washiriki wa harambee hiyo.
 Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi William Ole Nasha  akizungumza kwenye harambee hiyo.  Ole Nasha alimuwakilisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwenye harambee hiyo iliyofanyika kwa mafanikio makubwa!
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini  (TADB) Bw Francis Assenga akizungumza kwenye harambee hiyo.Benki hiyo ilitangaza nia yake ya kutenga sh milioni 600 kuwezesha miradi ya taasisi  ya CAWAT. 
Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi William Ole Nasha akipeana mkono wa pongezi na Meneja Uhusiano wa Mfuko wa pesheni wa PPF, Lulu Mengele ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wa mfuko huo kwenye harambee hiyo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...