Sensei Rumadha Fundi, mwakilishi wa Jundokan So Honbu Tanzania, na wanafunzi waandamizi toka " Jamhuri Kaizen Dojo  na Zanaki Dojo " za Dat es salaam wanakitarajiwa kupandishwa ngazi ya chama hicho baada ya semina ya 
(European Jundokan Gasshuku) Mnamo mwezi July 14 hadi  16, 2017. katika mji wa Marki,  nje kidogo ya mji wa Warsaw, Poland.
Hali kadhalika Sensei Rumadha amepewa mwaliko huo ikiwa ni sehemu ya kwenda kukutana  na walimu wakuu ( Masters) toka Okinawa,  Japan,  na kufanya mtihani wa shahada ya nne "Yondan" ya Goju Ryu chini ya mwenyekiti wake, Master Kancho Yoshihiro Miyazato. 
Maandalizi makubwa yanatarajiwa kwa wanafunzi wa Tanzania ambapo hatimaye watapandishwa ngazi za ualimu za " Sensei " mara baada ya  Sensei Rumadha kuwasili  nchini baada ya semina hiyo ya Poland.
 Sensei  Rumadha na wanafunzi wake wa wakilishi wa Tanzania Senpai Waheed na Senpai Jesse wakiwa mazoezi jijini Dar es salaam ni hivi karibuni. 
Sensei  Rumadha na wanafunzi wa Zanaki Dojo wakiwa mazoezi jijini Dar es salaam ni hivi karibuni. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...