Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe amewaagiza Viongozi wa Serikali Mkoani humo ngazi ya Wilaya hadi kata kuwa na madaftari ya kuwasajiri wakulima ifikapo Machi 31, mwaka huu.


Dkt. Kebwe ametoa agizo hilo Februari 22 mwaka huu wakati anatembelea kiwanda cha kuzalisha Mpunga cha KPL kilichopo katika Wilayani ya Kilombero ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tano aliyoifanya Wilayani humo.

Katika maelezo yake Dkt. Kebwe amesema zoezi la usajiri wa wafugaji pamoja na mifugo yao lazima liende sambamba na zoezi la usajiri wa wakulima kwa lengo lilelile la kupata takwimu halisi kwa Mkoa mzima na si kuwa na takwimu za mezani.

“Sambamba na kazi ambayo tuliianza mwaka jana mwezi wa sita ya utambuzi wa mifugo kazi ambayo inaendelea awamu ya pili, madftari ya wafugaji sehemu kubwa yameanza kuwepo wafugaji wanatambuliwa. Kwa hiyo vitu hivi viwili lazima viende sambamba hii inasaidia kutengeneza maoteo katika Halmashauri zetu. Huwezi kufanya maoteo bila kuwa na tax base” alisema Dkt. Kebwe

Mkuu huyo wa Mkoa ameonekana kuridhishwa na juhudi zinazooneshwa na baadhi ya wakulima hususani wa Wilaya ya Kilombero kujihusisha katika kilimo na kusema amejionea mwenyewe watu wamelima mashamba makubwa ingawa mvua zimechelewa kunyesha tofauti na maeneo mengine ambapo wamelima maeneo madogo.

Mkuu wa mkoa wa Morogoro Mh. Steven Kebwe akishiriki katika kazi ya kiwekea mifugo alama ikiwa ni utambuzi wa mifugo hiyo.
Ng’ombe ambao tayari wamesha wekewa alama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...