Prof. Ninatubu Mbora Lema
Ikulu, Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemteua Prof. Ninatubu Mbora
Lema kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
Tanzania (TAA).
Taarifa
iliyotolewa leo tarehe 22 Oktoba, 2016 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John
Kijazi imeeleza kuwa uteuzi huu umeanza tarehe 20 Oktoba, 2016.
Prof. Ninatubu
Mbora Lema anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Mhandisi Lambert Ndiwaita
aliyefariki dunia tarehe 20 Agosti, 2015.
Prof. Ninatubu
Mbora Lema ni Profesa Mshiriki Usimamizi wa Ujenzi, Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (Associate Professor of
Construction Management - University of Dar es Salaam).
Gerson
Msigwa
Mkurugenzi
wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es
Salaam
22 Oktoba,
2016
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...